Kitabu Maombi 16 jinsi ya kuomba maombi mbalimbali na kujibiwa na Mungu kimekuwa msaada mkubwa kwa wakristo wengi.Kimekuwa msaada katika kumwongoza Mkristo jinsi ya kuomba,kujisimamia na Neno la Mungu katika maombi ya kile siku na hata katika kujiombea mwenyewe pale unapohitaji msada wa Kiroho zaidi. Mpendwa/Mkristo akimshukuru Bwana kwa msaada mkubwa alioupata kupitia kitabu hichi lakini pia jinsi kilivyomsaidia kumwona Mungu zaidi na maisha yake kubadilika pia. Mbali na mwongozo wa kiroho kitabu hichi kimesaidia wengi kupokea uponyaji kwa magonjwa na vifungo mbalimbali walivyofungwa na adui kupitia maombi mbalimbali yaliyomo ndani ya kitabu. Tunamshukuru Bwana Yesu aliye hai kwa kuzidi fungua wengi na kuwaleta wengi katika Ufalme wake wa Mbinguni amina.